Showing posts with label Legal documents. Show all posts
Showing posts with label Legal documents. Show all posts

Friday, 26 August 2022

MAOMBI YA FARAGHA YA KUONGEZEWA MUDA

 KATIKA JAMUHURI YA MUUNGANO YA TANZANIA

KATIKA BARAZA LA ARDHI NA NYUMBA LA ILALA

LILILOPO JENGO LA MWALIMU

MAOMBI MADOGO NAMBA ____ YA MWAKA 2022

(Yanayotokana na maombi namba ......... ya mwaka 2022)

BAINA YA

XXX.............................................. MLETA MAOMBI

DHIDI

YYY ..............................MJIBU MAOMBI


MAOMBI YA FARAGHA

(Yanafanywa chini ya kifungu cha 14 cha sheria ya Ukomo wa muda sura ya 89 iliyofanyiwa mapitio mwaka 2019, na sheria nyingine yoyote itakayohusika)


PANDE ZOTE WANAOHUSIKA WAFIIKE, mbele ya Mheshimiwa..................Mwenyekiti wa Baraza katika chumba cha Mwenyekiti tarehe ......... mwezi wa ...... mwaka 2022, au katika muda utakaoamriwa, ambapo mwombaji atasikilizwa maombi yake kwa kupatiwa amri zifuatazo: -

1. Kwamba mahakama itoe ruhusa kwa mleta maombi kuongezewa muda ili afanye maombi ya kutengua hukumu ya upande mmoja iliyotolewa katika maombi namba....... la mwaka 2022.

2. Mahakama itoe nafuu nyingine yoyote kwa kwa kadiri itakavyo ona ni haki kutoa.

Maombi haya yanafanywa na  kwa sambamba sababu vigezo na sababu zilivotajwa katika kiapo cha mleta maombi XXX ambacho kimeambatanishwa katika maombi haya na sababu za ziada zitatolewa na mleta maombi wakati wa kusikilizwa maombi haya.

...........................................

MWENYEKITI


Yameletwa kusajilwa leo hii ...................... Siku ya mwezi wa ...................mwaka 2022.

...........................................

KARANI WA BARAZA


YAMEANDALIWA NA

XXX, MLETA MAOMBI,

S.L.P.

DAR ES SALAAM,

TANZANIA


NAKALA APATIWE

YYY, MJIBU MAOMBI

Wednesday, 17 August 2022

MKATABA WA KUPANGISHA NYUMBA

 

 Below is a swahili contract for leasing a house.

 

 

 

 

MKATABA WA KUPANGISHA NYUMBA

 

 

 

KATI YA

 

 

 

 

…….………………………………………………….

(MWENYE NYUMBA)

 

 

 

 

NA

 

 

 

 

 

………………………………………………………….

MPANGAJI

 

 

 

 

 

KATIKA NYUMBA ILIYOPO

 

………………………………………………………

 

 

 

 

 

 

MKATABA WA KUPANGISHA NYUMBA.

 

MKATABA huu umefanyika leo tarahe  ……….… mwezi wa ………….., mwaka ………………… kati ya Bwana ………………………………………wa Sanduku la Posta ………………………………………., kwa upande mmoja (ambaye katika mkataba huu ataitwa “MWENYE NYUMBA”), NA …………………………………………..… wa Sanduku la Posta ………………….. , …………………………. (ambaye katika mkataba huu ataitwa “MPANGAJI”.

 

KWA KUWA mwenye nyumba ni mmiliki halali wa nyumba yenye vyumba ………………………… vya kulala, sebule, choo na bafu, jiko, chumba cha kulia chakula iliyopo kwenye kitalu namba …………………………………, katika Manispaa ya .................... mkoani ....................

 na

 

KWA KUWA mpangaji amemwendea mwenye nyumba kwa nia ya kutaka kupangisha nyumba hiyo kwa muda wa kipindi cha mwaka mmoja kwa malipo ya kodi iliyokubaliwa katika mkataba huu na kwa mujibu wa masharti mengineyo yatakayoafikiwa kwenye mkataba huu; na

 

KWA KUWA mwenye nyumba mwenye nyumba amekubali kumpangisha mpangaji katika nyumba hiyo;

 

 

HIVYO BASI, MKATABA huu unashuhudia na kuthibitisha kama ifuatavyo:

 

1.        KWAMBA Mwenye nyumba amempangisha mpangaji nyumba hiyo iliyopo katika eneo lililotajwa hapo juu kwa kiasi cha kodi ya Tshs. ………………………………….. tu, (Tshs. ……………………….) kwa mwezi na kwamba fedha hizo zitalipwa kwa mkupuo kwa kwa kipindi chote cha ……………………………… cha mkataba huo yaani jumla ya Tshs. ………………………………tu (Tshs. …………………………).

 

2.        KWAMBA mpangaji ataanza kupanga nyumba hiyo kuanzia tarehe ……….. mwezi ………………. Mwaka ……………………………. ambapo mkataba huo utakoma.

 

3.        KWAMBA, ikiwa Mpangaji anatimiza masharti yote ya ulipaji kodi na mengineyo, Mwenye nyumba anampangisha mpangaji nyumba hiyo bila kumuingilia katika kipindi chote cha upangaji huo.

 

4.        KWAMBA Mpangaji anatakiwa azingatie usafi wa nyumba pamoja na mazingira yake na anatakiwa atumie nyumba hiyo kwa matumizi ya makazi tu na sio vinginevyo na yote haya yanafanyika pasipo kufanya shughuli nyingine yoyote katika nyumba hiyo ambacho kitakuwa ni kinyume cha sheria na taratibu za nchi.

 

5.        KWAMBA Mpangaji anatakiwa azingatie kulipa kodi kama inavyotakiwa na kuilipa kwa wakati kama ilivyokubaliwa katika mkataba huu.

  

6.        KWAMBA Mwenye nyumba, kwa wakati muafaka anayo haki ya kuingia katika nyumba hiyo pale inapobidi ili kukagua au kufanya ukarabati wa nyumba hiyo.

 

7.        KWAMBA Mpangaji anatakiwa aiweke nyumba hiyo anayopanga katika hali ya usafi wakati wote na kuhakikisha kwamba kuta na sehemu zingine za chumba haziharibiwi.

 

8.        KWAMBA Mpangaji anatakiwa alipie maji, umeme au simu katika nyumba hiyo kwa muda wote atakaopanga nyumnba hiyo na wakati wa kuondoka katika nyumba hii atahakikisha kuwa hataacha madeni yoyote yanayohusiana na umeme, maji au simu.

 

9.        KWAMBA Mpangaji haruhusiwi kufanya matengenezo au marekebisho yoyote katika nyumba hiyo aliyopanga bila idhini ya maandishi kutoka kwa mwenye nyumba kwa muda watakaokubaliana.

 

10.      KWAMBA Mpangaji haruhisiwi kukodisha nyumba hiyo aliyopanga kwa mtu mwingine yeyote bila ya idhini ya maandishi kutoka kwa Mwenye Nyumba, na ikiwa Mpangaji atashindwa kuendelea na Mkataba basi mpangaji atamrudishia nyumba mwenye nyumba.

 

11.      KWAMBA Mpangaji ahakikishe kwamba kwa wakati wote atakaokuwa kwenye nyumba hiyo hatawaghasi majirani wenzake kwa njia yoyote ile.

 

12.      KWAMBA Mpangaji amjulishe mwenye nyumba kwa maandishi mwanzo wa mwezi mmoja (1) wa mwisho wa mkataba huu endapo atapenda kuendelea na mkataba huu mara utakapokwisha.

 

13.      KWAMBA Mpangaji na Mwenye nyumba wanaweza kusitisha mkataba huu kwa kutoa taarifa kwa maandishi mwezi mmoja kabla.   

 

14.      KWAMBA Maneno “Mwenye Nyumba” na “Mpangaji” yatahusu familia, jamii na wategemea wa kila mmoja wao kwa madhumuni ya mkataba huu.

 

KWA USHUHUDA na UTHIBITISHO, mkataba huu umewekwa sahihi na Mwenye Nyumba na Mpangaji mbele ya mashahidi kama inavyoonyeshwa hapa chini:

 

 

 

IMETIWA SAHIHI na KUTOLEWA                     )

na ………………………….. leo hii                     )    ...................................

tarehe ….. mwezi ……….. mwaka ……….      )    MWENYE NYUMBA

 

Mbele ya:-

 

Jina:               ……………………………………

 

Wadhifa:       ……………………………………

 

Sahihi:- ……………………………………………

 

Tarehe:         ……………………………………

 

 

 

IMETIWA SAHIHI na KUTOLEWA                     )

na …………………………………. leo hii             )           ..................................

tarehe ….. mwezi ……….. mwaka ………..     )           MWENYE NYUMBA

 

Mbele ya:-

 

Jina:               ……………………………………

 

Wadhifa:       ……………………………………

 

Sahihi:- ……………………………………………

 

Tarehe:         ……………………………………

 

 

 

Umeandaliwa na:-

 

…………………………………..

S. L. Posta

Dar es Salaam

 

Mkataba wa mauziano ya eneo

MKATABA WA MAUZIANO YA SHAMBA

 

MAKUBALIANO HAYA YAMEFANYIKA siku ya tarehe _____ mwezi __________, Mwaka 2022

BAINA YA:

ndugu________________________ (mwenye kitambulisho cha taifa namba ___________________________)  wa sanduku la posta ___________ _______

na

ndugu ________________________ (mwenye kitambulisho cha taifa namba ___________________________), wa sanduku la posta ________ _______ambaye ndani ya mkataba huu watakua wanatajwa kama WAUZAJI; KWA UPANDE MMOJA

NA

Ndugu ___________________________ wa sanduku la posta _______, Dar es Salaam, ambaye ndani ya mkataba huu atakua anatajwa kama MNUNUZI. KWA UPANDE WA PILI

KWA KUWA:

a. WAUZAJI ndiye wamiliki halali wa eneo eneo linalouzwa lenye ukubwa wa __________________ ambalo lipo katika eneo la ____________, Kitongoji cha ________________________, Kata ya ________________________, Wilaya Ya ________________________, mkoa wa _______________________

b.   MNUNUZI kwa hiari yake mwenyewe ameridhia na ameamua kununua nyumba kama ilivyotajwa na Mkataba huu, na hasa baada ya kuikagua na kuridhika

WAHUSIKA WA MKATABA HUU WANAKUBALIANA YAFUATAYO:

1.      KWAMBA Wauzaji ni wamiliki halali wa eneo linalouzwa lenye ukubwa wa __________________ ambalo lipo katika eneo la ____________, Kitongoji cha ________________________, Kata ya ________________________, Wilaya Ya ________________________, mkoa wa ________________________na ambalo limetambuliwa na kuonyeshwa kwa Mnunuzi na mipaka yake yote mbele ya mashahidi waliotajwa na kuweka sahihi zao katika hati hii kama ilivyoonyeshwa hapa chini.

2.      KWAMBA Wauzaji wakiwa na akili timamu na kwa hiari zao wanamuuzia Mnunuzi eneo hilo lenye ukubwa wa ekari tano bei ya TZS__________________ (Shilingi ya Kitanzania __________________Tu)

3.      KWAMBA Wauzaji wanauza eneo hilo likiwa halina migogoro yoyote na haliko chini ya madai yoyote na kwamba umiliki wa Muuzaji wa shamba hilo haugombaniwi wala kubishaniwa na mtu yoyote.

4.      KWAMBA endapo Mnunuzi atapoteza umiliki wa shamba hilo kutokana na Muuzaji kutokuwa na umiliki halali na dhabiti au eneo hilo kuwa na mgogoro au migogoro ya umiliki imhusishayo au kumhusu Muuzaji kwa jinsi yoyote ile, basi Wauzaji watalazimika kumlipa Mnunuzi pesa zake zote alizomlipa kununua eneo hilo pamoja na riba na gharama ambazo Mnunuzi atakuwa ameingia kutokana na mgogoro au migogoro hiyo.

5.      KWAMBA Mnunuzi leo hii tarehe ya mkataba huu amewalipa wauzaji jumla ya TZS__________________ (Shilingi ya Kitanzania __________________Tu) ikiwa ni bei kamili ya mauzo ya eneo hilo na Wauzaji kwa mkataba huu wanakiri kupokea fedha hizo zote na hawana madai yoyote dhidi ya Mnunuzi.

6.      KWAMBA kwa mkataba huu Wauzaji wanamkabidhi Mnunuzi eneo hilo liwe katika milki yake moja kwa moja na hawataingilia umiliki wa Mnunuzi.

7.     KWAMBA maneno “Wauzaji” na “Mnunuzi” yatahusu familia, jamii na wategemea wa kila mmoja wao kwa madhumuni ya mkataba huu.

8.      KWAMBA migogoro yoyote itakayotokana na tafsiri ya Mkataba huu, au jambo jingine lolote litokanalo na Mkataba  huu au mauzo yaliyofanyika, litatatuliwa na pande mbili husika kwa namna itakavyopendekezwa na wahusika wenyewe,  isipokuwa pale utatuzi unaposhindikana, basi mgogoro au jambo hilo litatatuliwa na vyombo vinavyofahamika kisheria, kwa kutumia Sheria za Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania.

 NA INASHUHUDIWA kwamba wahusika katika mkataba huu wameingia mkataba huu siku hii kama inavyo onekana hapo chini:


Mkataba UMESAINIWA na

________________________, siku hii                                                          

ya tarehe ______mwezi wa_____________2022                         Saini ya Muuzaji

 


Mkataba UMESAINIWA na

________________________, siku hii                                                                                                                 

ya tarehe ______mwezi wa_____________2022                          Saini ya Muuzaji

                                                                                           

MBELE YA MASHAIDI

JINA LA SHAHIDI: ________________________

Sahihi: ___________________________                                                                        

Wadhifa: ________________________ 

Anuani: ______________________

Tarehe: _______________________

 

JINA LA SHAHIDI: ________________________

Sahihi: _________________________

Wadhifa:________________________

Anuani: ________________________

Tarehe: _________________________



Mkataba UMESAINIWA na

________________________________

ambaye ninamfahamu katika siku hii ya                             ____________________

tarehe 18 mwezi wa nane, 2022                                           Saini ya Muuzaji

 

MBELE YANGU

Sahihi:_________________________                              

Jina ___________________________                             

Anuani:________________________

Wadhifa _______________________