|
MKATABA WA MAUZIANO YA SHAMBA
|
MAKUBALIANO HAYA YAMEFANYIKA siku ya tarehe _____ mwezi __________,
Mwaka 2022
BAINA YA:
ndugu________________________ (mwenye kitambulisho cha taifa namba ___________________________) wa sanduku la posta ___________
_______
na
ndugu ________________________ (mwenye
kitambulisho cha taifa namba ___________________________), wa sanduku la posta ________
_______ambaye ndani ya mkataba huu watakua wanatajwa kama WAUZAJI; KWA UPANDE MMOJA
NA
Ndugu ___________________________ wa sanduku la posta
_______, Dar es Salaam, ambaye
ndani ya mkataba huu atakua anatajwa kama MNUNUZI.
KWA UPANDE WA PILI
KWA KUWA:
a. WAUZAJI ndiye wamiliki
halali wa eneo eneo linalouzwa lenye ukubwa wa __________________ ambalo lipo katika eneo la ____________, Kitongoji cha ________________________, Kata ya ________________________, Wilaya Ya ________________________, mkoa wa _______________________
b. MNUNUZI kwa hiari yake mwenyewe ameridhia na ameamua kununua nyumba kama ilivyotajwa
na Mkataba huu, na hasa baada ya kuikagua na kuridhika
WAHUSIKA WA MKATABA HUU WANAKUBALIANA YAFUATAYO:
1.
KWAMBA Wauzaji ni wamiliki halali wa eneo
linalouzwa lenye ukubwa wa __________________ ambalo lipo katika eneo la ____________,
Kitongoji cha ________________________, Kata ya ________________________, Wilaya Ya ________________________, mkoa wa ________________________na
ambalo limetambuliwa na kuonyeshwa kwa Mnunuzi na mipaka yake yote mbele ya
mashahidi waliotajwa na kuweka sahihi zao katika hati hii kama ilivyoonyeshwa
hapa chini.
2.
KWAMBA Wauzaji wakiwa na akili timamu na
kwa hiari zao wanamuuzia Mnunuzi eneo hilo lenye ukubwa wa ekari tano bei ya TZS__________________ (Shilingi ya Kitanzania
__________________Tu)
3.
KWAMBA Wauzaji wanauza eneo hilo likiwa
halina migogoro yoyote na haliko chini ya madai yoyote na kwamba umiliki wa
Muuzaji wa shamba hilo haugombaniwi wala kubishaniwa na mtu yoyote.
4.
KWAMBA endapo Mnunuzi atapoteza umiliki
wa shamba hilo kutokana na Muuzaji kutokuwa na umiliki halali na dhabiti au eneo
hilo kuwa na mgogoro au migogoro ya umiliki imhusishayo au kumhusu Muuzaji kwa
jinsi yoyote ile, basi Wauzaji watalazimika kumlipa Mnunuzi pesa zake zote
alizomlipa kununua eneo hilo pamoja na riba na gharama ambazo Mnunuzi atakuwa
ameingia kutokana na mgogoro au migogoro hiyo.
5.
KWAMBA Mnunuzi leo hii tarehe ya mkataba
huu amewalipa wauzaji jumla ya TZS__________________ (Shilingi ya Kitanzania __________________Tu) ikiwa ni bei kamili ya mauzo ya eneo
hilo na Wauzaji kwa mkataba huu wanakiri kupokea fedha hizo zote na hawana
madai yoyote dhidi ya Mnunuzi.
6.
KWAMBA kwa mkataba huu Wauzaji wanamkabidhi
Mnunuzi eneo hilo liwe katika milki yake moja kwa moja na hawataingilia umiliki
wa Mnunuzi.
7. KWAMBA maneno “Wauzaji” na “Mnunuzi”
yatahusu familia, jamii na wategemea wa kila mmoja wao kwa madhumuni ya mkataba
huu.
8.
KWAMBA migogoro yoyote itakayotokana na
tafsiri ya Mkataba huu, au jambo jingine lolote litokanalo na Mkataba huu au mauzo yaliyofanyika, litatatuliwa na
pande mbili husika kwa namna itakavyopendekezwa na wahusika wenyewe, isipokuwa pale utatuzi unaposhindikana, basi
mgogoro au jambo hilo litatatuliwa na vyombo vinavyofahamika kisheria, kwa
kutumia Sheria za Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania.
NA INASHUHUDIWA kwamba
wahusika katika mkataba huu wameingia mkataba huu siku hii kama inavyo onekana
hapo chini:
Mkataba UMESAINIWA na
________________________, siku hii
ya tarehe ______mwezi wa_____________2022 Saini ya Muuzaji
Mkataba UMESAINIWA na
________________________, siku hii
ya tarehe ______mwezi wa_____________2022 Saini ya Muuzaji
MBELE YA MASHAIDI
JINA LA SHAHIDI: ________________________
Sahihi: ___________________________
Wadhifa: ________________________
Anuani: ______________________
Tarehe: _______________________
JINA LA SHAHIDI: ________________________
Sahihi: _________________________
Wadhifa:________________________
Anuani: ________________________
Tarehe: _________________________
Mkataba UMESAINIWA na
________________________________
ambaye ninamfahamu katika siku hii ya ____________________
tarehe 18 mwezi wa nane, 2022 Saini ya
Muuzaji
MBELE YANGU
Sahihi:_________________________
Jina ___________________________
Anuani:________________________
Wadhifa
_______________________