Showing posts with label mkataba wa upangishaji. Show all posts
Showing posts with label mkataba wa upangishaji. Show all posts

Tuesday, 20 May 2025

MKATABA WA KUKODISHA NYUMBA

MKATABA WA KUKODISHA NYUMBA
Kati ya:
A. MKODISHAJI (Mwenye Nyumba):
Jina Kamili: _________________________________________________________
Anwani: ____________________________________________________________
Nambari ya Simu: ____________________
Kitambulisho (NIDA/Passport): ____________________

B. MKODI (Mtumiaji wa Nyumba):
Jina Kamili: _________________________________________________________
Anwani: ____________________________________________________________
Nambari ya Simu: ____________________
Kitambulisho (NIDA/Passport): ____________________

Mali Yenye Kukodishwa:
Anwani Kamili: ______________________________________________________
Aina ya Mali (Nyumba/Ghorofa/Rumu): __________________________________

SEHEMU YA 1: MADA NA SIFA ZA MKATABA
Lengo la Mkataba: Mkodishaji anakubali kukodisha na mkodi anakubali kukodi mali iliyoainishwa hapo juu.

Muda wa Ukodishaji:

Mwanzo: Tarehe ______ /______ /______

Mwisho: Tarehe ______ /______ /______

Mkataba huu unaweza kusitishwa kwa maelewano au kwa mujibu wa masharti yaliyoorodheshwa hapa chini.

SEHEMU YA 2: MALIPO NA DENI
Kodi ya Mwezi:

Kodi: _____________ (TSh/KSh/USD) kwa mwezi.

Malipo yatafanyika kila mwezi siku ya ______.

Amana (Deposit): _____________ (kawaida sawa na kodi 1-2) itarudishwa mwisho wa mkataba ikiwa hakuna uharibifu au deni.

Faini za Ucheleweshaji:

Kodi isipolipwa kwa siku ______, fidia ya ______% ya kodi ya mwezi itatumika.

SEHEMU YA 3: HAKI NA WAJIBU WA MKODI
Matumizi ya Mali:

Kwa makazi pekee (au biashara ikiwa imeidhinishwa).

Hakuruhusiwi kukodishwa tena (sublet) bila idhini ya mkodishaji.

Matengenezo:

Mkodi atalipa gharama za uharibifu uliotokana na matumizi yasiyo ya kawaida.

Mkodishaji atasimamia matengenezo ya kawaida (mifumo ya maji, umeme, n.k.).

SEHEMU YA 4: HAKI NA WAJIBU WA MKODISHAJI
Haki ya Kuingia:

Mkodishaji anaweza kuingia kwenye mali kwa taarifa ya siku ______ kwa ajili ya ukaguzi au matengenezo.

Usalama wa Mkodi:

Mkodishaji atahakikisha mali iko salama na inakidhi vigezo vya kikao.

SEHEMU YA 5: KUKOMEA AU KUVUNJA MKATABA
Mkataba wa Muda Mrefu:

Ikiwa mkodi ataendelea kukaa baada ya mwisho wa mkataba, mkataba utaendelea kwa mipango ya kila mwezi.

Kuvunja Mapema:

Ikiwa mkodi atahitaji kuondoka mapema, anapaswa kutoa notisi ya siku ______ na kulipa fidia ya ______ (mwezi/miezi) ya kodi.

Mkodishaji anaweza kumfukuza mkodi kwa ukiukwaji wa masharti au kukosa malipo kwa mwezi ______ mfululizo.

SEHEMU YA 6: SHERIA NA MIZANI
Mamlaka ya Sheria: Mkataba huu utatawaliwa na sheria za ______ (nchi).

Mizani: Mashitaka yote yatatatuliwa kwa maridhiano au mahakama za ______.

SEHEMU YA 7: SAHIHI NA MASHUHUDA
Mkodishaji:
Sahihi: ________________________
Tarehe: ______ /______ /______

Mkodi:
Sahihi: ________________________
Tarehe: ______ /______ /______

Mashahidi (2):

Jina: ________________________ Sahihi: __________

Jina: ________________________ Sahihi: __________

Wednesday, 17 August 2022

MKATABA WA KUPANGISHA NYUMBA

 

 Below is a swahili contract for leasing a house.

 

 

 

 

MKATABA WA KUPANGISHA NYUMBA

 

 

 

KATI YA

 

 

 

 

…….………………………………………………….

(MWENYE NYUMBA)

 

 

 

 

NA

 

 

 

 

 

………………………………………………………….

MPANGAJI

 

 

 

 

 

KATIKA NYUMBA ILIYOPO

 

………………………………………………………

 

 

 

 

 

 

MKATABA WA KUPANGISHA NYUMBA.

 

MKATABA huu umefanyika leo tarahe  ……….… mwezi wa ………….., mwaka ………………… kati ya Bwana ………………………………………wa Sanduku la Posta ………………………………………., kwa upande mmoja (ambaye katika mkataba huu ataitwa “MWENYE NYUMBA”), NA …………………………………………..… wa Sanduku la Posta ………………….. , …………………………. (ambaye katika mkataba huu ataitwa “MPANGAJI”.

 

KWA KUWA mwenye nyumba ni mmiliki halali wa nyumba yenye vyumba ………………………… vya kulala, sebule, choo na bafu, jiko, chumba cha kulia chakula iliyopo kwenye kitalu namba …………………………………, katika Manispaa ya .................... mkoani ....................

 na

 

KWA KUWA mpangaji amemwendea mwenye nyumba kwa nia ya kutaka kupangisha nyumba hiyo kwa muda wa kipindi cha mwaka mmoja kwa malipo ya kodi iliyokubaliwa katika mkataba huu na kwa mujibu wa masharti mengineyo yatakayoafikiwa kwenye mkataba huu; na

 

KWA KUWA mwenye nyumba mwenye nyumba amekubali kumpangisha mpangaji katika nyumba hiyo;

 

 

HIVYO BASI, MKATABA huu unashuhudia na kuthibitisha kama ifuatavyo:

 

1.        KWAMBA Mwenye nyumba amempangisha mpangaji nyumba hiyo iliyopo katika eneo lililotajwa hapo juu kwa kiasi cha kodi ya Tshs. ………………………………….. tu, (Tshs. ……………………….) kwa mwezi na kwamba fedha hizo zitalipwa kwa mkupuo kwa kwa kipindi chote cha ……………………………… cha mkataba huo yaani jumla ya Tshs. ………………………………tu (Tshs. …………………………).

 

2.        KWAMBA mpangaji ataanza kupanga nyumba hiyo kuanzia tarehe ……….. mwezi ………………. Mwaka ……………………………. ambapo mkataba huo utakoma.

 

3.        KWAMBA, ikiwa Mpangaji anatimiza masharti yote ya ulipaji kodi na mengineyo, Mwenye nyumba anampangisha mpangaji nyumba hiyo bila kumuingilia katika kipindi chote cha upangaji huo.

 

4.        KWAMBA Mpangaji anatakiwa azingatie usafi wa nyumba pamoja na mazingira yake na anatakiwa atumie nyumba hiyo kwa matumizi ya makazi tu na sio vinginevyo na yote haya yanafanyika pasipo kufanya shughuli nyingine yoyote katika nyumba hiyo ambacho kitakuwa ni kinyume cha sheria na taratibu za nchi.

 

5.        KWAMBA Mpangaji anatakiwa azingatie kulipa kodi kama inavyotakiwa na kuilipa kwa wakati kama ilivyokubaliwa katika mkataba huu.

  

6.        KWAMBA Mwenye nyumba, kwa wakati muafaka anayo haki ya kuingia katika nyumba hiyo pale inapobidi ili kukagua au kufanya ukarabati wa nyumba hiyo.

 

7.        KWAMBA Mpangaji anatakiwa aiweke nyumba hiyo anayopanga katika hali ya usafi wakati wote na kuhakikisha kwamba kuta na sehemu zingine za chumba haziharibiwi.

 

8.        KWAMBA Mpangaji anatakiwa alipie maji, umeme au simu katika nyumba hiyo kwa muda wote atakaopanga nyumnba hiyo na wakati wa kuondoka katika nyumba hii atahakikisha kuwa hataacha madeni yoyote yanayohusiana na umeme, maji au simu.

 

9.        KWAMBA Mpangaji haruhusiwi kufanya matengenezo au marekebisho yoyote katika nyumba hiyo aliyopanga bila idhini ya maandishi kutoka kwa mwenye nyumba kwa muda watakaokubaliana.

 

10.      KWAMBA Mpangaji haruhisiwi kukodisha nyumba hiyo aliyopanga kwa mtu mwingine yeyote bila ya idhini ya maandishi kutoka kwa Mwenye Nyumba, na ikiwa Mpangaji atashindwa kuendelea na Mkataba basi mpangaji atamrudishia nyumba mwenye nyumba.

 

11.      KWAMBA Mpangaji ahakikishe kwamba kwa wakati wote atakaokuwa kwenye nyumba hiyo hatawaghasi majirani wenzake kwa njia yoyote ile.

 

12.      KWAMBA Mpangaji amjulishe mwenye nyumba kwa maandishi mwanzo wa mwezi mmoja (1) wa mwisho wa mkataba huu endapo atapenda kuendelea na mkataba huu mara utakapokwisha.

 

13.      KWAMBA Mpangaji na Mwenye nyumba wanaweza kusitisha mkataba huu kwa kutoa taarifa kwa maandishi mwezi mmoja kabla.   

 

14.      KWAMBA Maneno “Mwenye Nyumba” na “Mpangaji” yatahusu familia, jamii na wategemea wa kila mmoja wao kwa madhumuni ya mkataba huu.

 

KWA USHUHUDA na UTHIBITISHO, mkataba huu umewekwa sahihi na Mwenye Nyumba na Mpangaji mbele ya mashahidi kama inavyoonyeshwa hapa chini:

 

 

 

IMETIWA SAHIHI na KUTOLEWA                     )

na ………………………….. leo hii                     )    ...................................

tarehe ….. mwezi ……….. mwaka ……….      )    MWENYE NYUMBA

 

Mbele ya:-

 

Jina:               ……………………………………

 

Wadhifa:       ……………………………………

 

Sahihi:- ……………………………………………

 

Tarehe:         ……………………………………

 

 

 

IMETIWA SAHIHI na KUTOLEWA                     )

na …………………………………. leo hii             )           ..................................

tarehe ….. mwezi ……….. mwaka ………..     )           MWENYE NYUMBA

 

Mbele ya:-

 

Jina:               ……………………………………

 

Wadhifa:       ……………………………………

 

Sahihi:- ……………………………………………

 

Tarehe:         ……………………………………

 

 

 

Umeandaliwa na:-

 

…………………………………..

S. L. Posta

Dar es Salaam